• HABARI MPYA

    Monday, July 27, 2015

    ALEXIS SANCHEZ ANAVYOJIFUA KIBINAFSI KUJIWEKA FITI KABLA YA KUREJEA ARSENAL

    BAADA ya kushinda Kombe la Copa America na wenyeji Chile, Alexis Sanchez alichukua mapumziko- lakini sasa ameanza maandalizi ya msimu mpya.
    Sanchez aliyepewa ruhusa ya mapumziko zaidi na kocha wa Arsenal, Arsene Wenger ameanza kufanya mazoezi binafasi kujiweka fiti na ameposti picha kwenye akaunti yake ya Instagram akiwa anajifua vikali ufukweni nchini kwao.
    Mchezaji huyo aliyeipa The Gunners Kombe la FA katika msimu wake wa kwanza, atakosa mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Chelsea Agosti 2 na hatakuwepo pia katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya England dhidi ya West Ham Agosti 9.
    Alexis Sanchez akiwa ufukweni mwa bahari akijifua vikali kujiweka fiti PICHA ZAIDI GONGA HAPA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ALEXIS SANCHEZ ANAVYOJIFUA KIBINAFSI KUJIWEKA FITI KABLA YA KUREJEA ARSENAL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top