• HABARI MPYA

    Monday, July 27, 2015

    MAN UNITED YASAJILI KIPA LA ARGENTINA, VALDES ATUPIWA VIRAGO RASMI

    Kipa Sergio Romero akiwa ameshika jezi ya Manchester United baada ya kukamilisha usajili wake jana PICHA ZAIDI GONGA HAPA

    WAPYA WALIOSAJILIWA MANCHESTER UNITED 

    Memphis Depay, PSV - Pauni Milioni 25
    Morgan Schneiderlin, Southampton - Pauni Milioni 25
    Bastian Schweinsteiger, B.Munich - Pauni Milioni 15
    Matteo Darmian, Torino - Pauni Milioni 12
    Sergio Romero - huru
    KLABU ya Manchester United imefanikiwa kumsajili kipa Muargentina, Sergio Romero kwa Mkataba wa miaka mitatu.
    Mlinda mlango huyo mwenye umri wa miaka 28 alikuwa huru na amechukuliwa kuziba nafasi ya Victor Valdes aliyekuwa kipa wa pili, ambaye sasa anaondoka.
    Romero alicheza chini ya Louis van Gaal klabu ya AZ Alkmaar wakati wanabeba ubingwa wa Ligi Kuu ya Uholanzi, maarufu kama Eredivisie mwaka 2009 na Muargentina huyo mara moja anaungana na wachezaji wenzake katika kambi ya kujiandaa na msimu nchini Marekani.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED YASAJILI KIPA LA ARGENTINA, VALDES ATUPIWA VIRAGO RASMI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top