Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
YANGA SC haijawajumuisha Mudathir Khamis, Rajab Zahir, Edward Charles na Hussein Javu katika kikosi chake cha wachezaji 20, kwa ajili ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame iliyoanza jana Dar es Salaam.
Kipa Mudathir amesajiliwa kutoka KMKM ya Zanzibar, wakati Zahir, Charles na Javu walikuwepo kwenye kikosi cha Yanga SC msimu uliopita.
Yanga SC ilianza vibaya kwa kufungwa mabao 2-1 na Gor Mahia ya Kenya katika mchezo wa ufunguzi wa Kundi A Uwanja wa Taifa, Dar e Salaam.
Na makocha wa timu hiyo, Mholanzi, Hans van der Pluijm na mzalendo Charles Boniface Mkwasa wamewaacha Zahir, Charles na Javu katika kikosi cha Kagame.
Majina ambayo Yanga SC imewasilisha Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kwa ajili ya Kagame ya 2015 ni makipa; Ally Mustafa na Deo Munishi ‘Dida’.
Mabeki ni Nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Juma Abdul, Kevin Yondani, Joseph Zutah, Oscar Joshua, Mwinyi Haji na Pato Ngonyani.
Viungo ni Mbuyu Twite, Simon Msuva, Andrey Coutinho, Haruna Niyonzima, Salum Telela, Deus Kaseke na Godfrey Mwashiuwa, wakati washambuliaji ni Amisi Tambwe, Kpah Sherman, Malimi Busungu na Donald Ngoma.
Yanga SC itashuka tena dimbani Jumatano kumenyana na Telecom ya Djibouti Saa 10: 00 jioni mchezo ambao utatanguliwa na mechi kati ya Khartoum na KMKM na KCCA na Adama City.
YANGA SC haijawajumuisha Mudathir Khamis, Rajab Zahir, Edward Charles na Hussein Javu katika kikosi chake cha wachezaji 20, kwa ajili ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame iliyoanza jana Dar es Salaam.
Kipa Mudathir amesajiliwa kutoka KMKM ya Zanzibar, wakati Zahir, Charles na Javu walikuwepo kwenye kikosi cha Yanga SC msimu uliopita.
Yanga SC ilianza vibaya kwa kufungwa mabao 2-1 na Gor Mahia ya Kenya katika mchezo wa ufunguzi wa Kundi A Uwanja wa Taifa, Dar e Salaam.
Yanga SC ilianza vibaya kwa kufungwa 2-1 na Gor Mahia jana |
Na makocha wa timu hiyo, Mholanzi, Hans van der Pluijm na mzalendo Charles Boniface Mkwasa wamewaacha Zahir, Charles na Javu katika kikosi cha Kagame.
Majina ambayo Yanga SC imewasilisha Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kwa ajili ya Kagame ya 2015 ni makipa; Ally Mustafa na Deo Munishi ‘Dida’.
Mabeki ni Nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Juma Abdul, Kevin Yondani, Joseph Zutah, Oscar Joshua, Mwinyi Haji na Pato Ngonyani.
Viungo ni Mbuyu Twite, Simon Msuva, Andrey Coutinho, Haruna Niyonzima, Salum Telela, Deus Kaseke na Godfrey Mwashiuwa, wakati washambuliaji ni Amisi Tambwe, Kpah Sherman, Malimi Busungu na Donald Ngoma.
Yanga SC itashuka tena dimbani Jumatano kumenyana na Telecom ya Djibouti Saa 10: 00 jioni mchezo ambao utatanguliwa na mechi kati ya Khartoum na KMKM na KCCA na Adama City.
John Bocco (kushoto) akiwania mpira dhidi ya mabeki wa KCCA |
Mshambuliaji Mtanzania wa KCCA, Shaaban Kondo (kushoto) akipambana na beki wa Azam FC, Serge Wawa Pascal |
Beki wa Azam FC, Erasto Nyoni (kulia) akimtoka beki wa KCCA, Hakim Senkumba |
Kiungo wa Azam FC, Salum Abubakar 'Sure Boy', Hakim Sekumba |
0 comments:
Post a Comment