• HABARI MPYA

    Sunday, July 05, 2015

    YANGA SC KUJIPIMA KWA KMKM JUMATANO KUJUA UBAVU WAKE KABLA YA KAGAME

    Yanga SC kwa sasa wanafanya mazoezi ufukweni
    YANGA SC watamenyana na KMKM ya Zanzibar Jumatano Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na baada ya hapo wataingia kambini kujiandaa na michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame.
    Kipute cha Kagame kinatarajiwa kuanza Julai 18, mwaka huu na zote Yanga SC na KMKM zitacheza michuano hiyo, zikiwa zimepangwa pamoja Kundi A na Gor Mahia ya Kenya, Telecom ya Somalia na Khartoum ya Sudan.
    Kundi B kuna APR ya Rwanda, Al Shandy ya Sudan, LLB ya Burundi na Elman ya Somalia, wakati Kundi C kuna Azam, Malakia ya Sudan Kusini, KCC  ya Uganda na Adama City ya Ethiopia.
    Jumamosi, Yanga SC watacheza mchezo mwingine wa kirafiki dhidi ya kombaini ya Polisi Tanzania inayojiandaa kwa michuano ya Majeshi ya SADC.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA SC KUJIPIMA KWA KMKM JUMATANO KUJUA UBAVU WAKE KABLA YA KAGAME Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top