| Sanchez akiwa ameinua Kombe akishangilia na wenzake usiku huu |
Baada ya sare ya 0-0 ndani ya dakika 120, mshambuliaji wa Arsenal ya England, Alexis Sanchez alifunga penalti ya nne ya Chile na kumaliza mchezo, baada ya Gonzalo Higuain na Ever Banega kukosa mfululizo mikwaj yao.
Waliofunga penalti za Chile mbali na Sanchez wengine ni Charles Aranguiz, Arturo Vidal na Matias Fernandez, wakati Lionel Messi alifunga penalti pekee ya Argentina.
Mfungaji wa penalti ya ushindi, Sanchez akiwa amevua jezi yake kukimbia kushangilia PICHA ZAIDI GOGA HAPA
Hii inakuwa fainali ya pili mfululizo ya michuano mikubwa Argentina inapoteza, baada ya awali kufungwa na Ujerumani katika fainali ya Kombe la Dunia katikati ya mwaka jana.


.png)
0 comments:
Post a Comment