• HABARI MPYA

    Tuesday, March 05, 2024

    NAMUNGO FC YAICHAPA KAGERA SUGAR 1-0 MAJALIWA


    BAO pekee la Ibrahim Abdallah dakika ya 31 limeipa Namungo FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Kagera Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.
    Namungo FC inafikisha pointi 23 katika mchezo wa 19 na kupanda nafasi ya saba, wakati Kagera Sugar inabaki na pointi zake 23 za mechi 20, ikishukia nafasi ya tisa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NAMUNGO FC YAICHAPA KAGERA SUGAR 1-0 MAJALIWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top