AFISA Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdulkarim Amin ‘Popat’ amepewa onyo kali kwa kuingia kwenye chumba cha kubadilishia nguo cha timu yao na kuzungumza na wachezaji wake muda mfupi kabla ya mechi.
Popat anatuhumiwa kufanya hivyo kabla ya mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara dhidi ya Dodoma Jiji FC Machi 3 Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam - Azam FC ikishinda 4-1.
Kuna adhabu zaidi zikiwemo za faini kwa klabu yake pamoja na wapinzani wao, Simba na Yanga kutokana na makosa mbalimbali ya kikanuni ikiwemo imani za kishirikina.
0 comments:
Post a Comment