MWANACHAMA wa muda mrefu wa Yanga na aliyekuwa mfanyakazi wa klabu hiyo, Meneno Hussein amefariki dunia leo nyumbani kwao Jijini Dodoma baada ya kusumbuliwa na maradhi.
Maneno alifahamika Yanga miaka ya 1980 akianza kama mpenzi aliyejitolea kusaidia timu kifedha, kabla ya baadaye kupangishwa eneo la biashara ya vinywaji makao makuu ya klabu, Jangwani.
Kufuatia kufungwa kwa Kaunta ya vinywaji klabuni, Maneno akahamia kwenye utumishi wa klabu kwanza kwa kujitolea kama mmoja msimamizi wa mapato na baadaye kuajiriwa kama mlinzi wa kambi ya timu.
Mungu ampumzishe kwa amani Maneno Hussein. Amín.
0 comments:
Post a Comment