TIMU ya Liverpool imetanguliza mguu mmoja hatua ya Robó Fainali ya UEFA Europa League baada ya ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya wenyeji, Sparta Prague usiku wa Alhamisi Uwanja wa Epet Arena Jijini Prague, Jamhuri y Czech.
Mabao ya Liverpool yamefungwa na Alexis Mac Allister dakika ya sita, Darwin Núñez mawili, dakika ya 25 na 45, Luis Diaz dakika ya 53 na Dominik Szoboszlai dakika ya 90.
Bao pekee la wenyeji, Sparta Prague alijifunga beki wa Liverpool, Conor Bradley dakika ya 46 na timu hizo zitarudiana Alhamisi ya Machi 14 Uwanja wa Anfield.
0 comments:
Post a Comment