• HABARI MPYA

    Saturday, June 04, 2022

    KILIMANJARO QUEENS YATOSHANA NGUVU NA ETHIOPIA, 2-2 NJERU


    TIMU ya wanawake ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Queens imetoa sare ya kufungana mabao 2-2 na Ethiopia katika mechi yake ya pili ya michuano ya CECAFA Challenge leo Uwanja wa FTC Njeru nchini Uganda.
    Mabao ya Kilimanjaro Queens yamefungwa na Opa Clement Sanga dakika ya 24 na Enekia Kasonga ‘Lunyamila’ dakika ya 77 na sasa wanafikisha pointi nne kufuatia ushindi wa 2-0 dhidi ya Sudan Kusini kwenye mechi ya kwanza juzi.
    Mechi nyingine leo, Sudan Kusini iliilaza Zanzibar Queens 1-0, hicho kikiwa kipigo cha pili kwao baada ya awali kufungwa 5-0 na Ethiopia katika mechi ya kwanza.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KILIMANJARO QUEENS YATOSHANA NGUVU NA ETHIOPIA, 2-2 NJERU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top