• HABARI MPYA

    Wednesday, June 08, 2022

    STARS YACHAPWA 2-0 NA ALGERIA DAR KUFUZU AFCON


    TANZANIA imejiwekea ukungu kwenye safari yake ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani Ivory Coast baada ya kuchapwa mabao 2-0 na Algeria usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. 
    Mabao ya Algeria yamefungwa na Amir Selmane Ramy Bensebaïni dakika ya 45 na ushei na M. Amoura dakika ya 89 na kwa matokeo hayo Algeria inafikisha pointi sita na kuendelea kuongozi kundi F kufuatia ushindi wa 2-0 kwenye mechi ya kwanza dhidi ya Uganda Jijini Algiers Jumamosi.
    Taifa Stars baada ya sare ya 1-1 ugenini na Niger sasa ni ya tatu. Niger baada ya sare ya 1-1 na Uganda leo Jijini Kampala inapanda nafasi ya pili na Uganda sasa inashika mkia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: STARS YACHAPWA 2-0 NA ALGERIA DAR KUFUZU AFCON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top