TIMU ya Azam FC imefanikiwa kukata tiketi ya kucheza Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kumaliza nafasi ya tatu kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara kufuatia ushindi wa 4-1 dhidi ya Biashara United leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Ilikuwa siku nzuri kwa mshambuliaji Mkongo, Idris Mbombo aliyefunga mabao matatu, huku bao lingine likifungwa na Never Tigere.
0 comments:
Post a Comment