• HABARI MPYA

    Tuesday, June 14, 2022

    GOLDEN STATE YAICHAPA BOSTON GAME 5 NBA

    KATIKA Ligi ya mpira wa Kikapu nchini Marekani, Golden State Warriors imeifunga Boston Celtics 104-94 Alfajiri ya leo na sasa wanaongoza kwa series 3-2 kuelekea Game 6 Alhamisi.
    Andrew Wiggins alifunga pointi 26 na rebounds 13, Klay Thompson pointi 21, Stephen Curry pointi 16 na assists nane na kama Celtics watashinda Alhamisi watarudi Bay Area kwa Game 7 Jumapili.
    Mechi zote tano hadi sasa zimeamuliwa kwa pointi 10 au zaidi.

    MATOKEO YA MECHI ZILIZOPITA NA RATIBA;
    June 2: Boston vs. Golden State, ​(120-108)
    June 5: Boston vs. Golden State, ​(88-107)
    June 8: Golden State vs. Boston ​(116-100)
    June 10: Golden State vs. Boston, ​(107 – 97)
    June 13: Boston vs. Golden State, ​(94-104)
    June 16: Golden State vs. Boston, 9 ET, ABC
    June 19: Boston vs. Golden State, 8 ET, ABC (wakilingana tena).

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: GOLDEN STATE YAICHAPA BOSTON GAME 5 NBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top