DROO ya Ligi Kuu ya Vijana chini ya umri wa miaka 20 imechezeshwa leo studio za AzamTv, Tabata Jijini Dar es Salaam na mabingwa watetezi, Mtibwa Sugar wameoangwa Kundi B pamoja na Dodoma Jiji, Mbeya Kwanza na Ruvu Shooting.
Kundi A linaundwa na Simba, Polisi Tanzania, Biashara United na Namungo FC, wakati Kundi C kuna Azam FC, Mbeya City, Coastal Union na Tanzania Prisons na Kundi D wapo washindi wa pili wa msimu uliopita, Yanga, Geita Gold, KMC na Kagera Sugar.
0 comments:
Post a Comment