TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imendoka leo kwenda Benin kwa ndege ya kukodi kwa ajili ya mchezo wake wa kwanza Kundi F kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) dhidi ya Niger Juni 4 Uwanja wa L'Amitié mjini Cotonou.
Baada ya hapo, Taifa Stars itarejea nyumbani kwa mchezo wa pili wa Kundi F dhidi ya Algeria Juni 8 Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam kuwania tiketi ya Ivory Coast 2023.
0 comments:
Post a Comment