• HABARI MPYA

    Tuesday, June 07, 2022

    KIINGILIO TAIFA STARS NA ALGERIA NI SH 3,000 KESHO DAR


    KIINGILIO cha chini katika mchezo wa Kundi F kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwakani nchini Ivory Coast baina ya wenyeji, Tanzania na Algeria ni Sh. 3,000.
    Bei hiyo ni kwa majukwaa ya mzunguko, wakati kwa VIP A, B na C ni Sh. 5,000.
    Ikumbukwe mechi za kwanza za kuwania tiketi ya Ivory Coast, wakiwa nyumbani Jijini Algiers, Algeria waliichapa Uganda 2-0 na Taifa Stars wakiwa ugenini Jijini Cotonou nchini Benin, walitoa sare ya 1-1 na Niger.
    Mbali na Stars na Algeria kumenyana kesho Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam, jirani zao, Uganda watakuwa wenyeji wa Niger Jijini Kampala.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KIINGILIO TAIFA STARS NA ALGERIA NI SH 3,000 KESHO DAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top