MSHAMBULIAJI wa Napoli ya Itali, Victor Osimhen jana amefunga manne Nigeria ikiibuka na ushindi wa rekodi kwenye historia ya AFCON mabao 10 -0 dhidi ya Sao Tome e Principe Uwanja wa Agadir nchini Morocco.
Katika mchezo huo wa kuwania tiketi ya AFCON ya mwakani nchini Ivory Coast, mabao mengine ya Super Eagles yalifungwa Terem Moffi mawili, Moses Simon, Oghenekaro Etebo, Ademola Lookman na Emmanuel Dennis kwa penalti.
0 comments:
Post a Comment