• HABARI MPYA

    Friday, June 17, 2022

    GOLDEN STATE NDIO MABINGWA NBA 2022


    TIMU ya Golden State Warriors ya  San Francisco imefanikitwa kutwaa taji la Ligi ya Mpira wa Kikapu Marekani (NBA) baada ya ushindi wa pointi 103-90 dhidi ya wenyeji, Boston Celtics katika mechi ya sita ukumbi wa TD Garden Arena, Boston.
    Golden State Warriors wanakuwa Mabingwa wa NBA katika msimu wa 75 kwa ushindi wa jumla wa michezo 4-2, pongezi kwa Stephen Curry aliyetoa mchango mkubwa kwa timu yake msimu huu ikishinda taji la saba baada ya awali kutwaa 1947, 1956, 1975, 2015, 2017 na 2018.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: GOLDEN STATE NDIO MABINGWA NBA 2022 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top