IMEWEKWA AGOSTI 20, 2013 SAA 5: 55 USIKU
SI kitu ambacho unaweza kuwaona makocha wa Ligi Kuu ya England wakifanya. Vema, si mbele ya kamera, popote.
Picha za kuzindua msimu za Bayern Munich, zinawaonyesha mabingwa hao wa Ulaya wakionja pombe aina ya Oktoberfest baada ya kuanza msimu kwa kishindo.
Timu nje: Wachezaji wa Munich wakiwa katika picha ya pamoja na makocha wao wakifurahia Oktoberfest
Mambo hayo: Kocha Pep Guardiola (mbele kushoto) na Mspanyola, Javi Martinez (chini kulia) wakifurahia Paulaner
Mtungi: Mabingwa wa Ujerumani na Ulaya wakifurahia mwanzo mzuri Bundesliga
Kocha mpya, Pep Guardiola aliyehamia Ujerumani kutoka Hispania, anaonekana aliye vizuri tu akifurahia Paulaner lager, akiwa na kikosi chake katika vazi la asili la Ujerumani.
Ni mavazi ambayo kwa watu kama Bastian Schweinsteiger na Phillip Lahm wameonekana mara kadhaa wakiwa wamevaa kabla, lakini kwa watu wapya Guardiola, Thiago Alcantara na Mario Gotze, hii ilikuwa mara ya kwanza na walipendeza.
Guardiola ameanza msimu kwa kipigo cha mabao 4-2 katika Super Cup ya Ujerumani kutoka kwa Dortmund, lakini akashinda mechi mbili mfululizo za Bundesliga, 3-1 dhidi ya Borussia Monchengladback na 1-0 dhidi ya Eintracht Frankfurt Jumamosi.
Mtu mpya: Guardiola (kushoto) akifurahia kaka ilivyo kwa mchezaji mpya Mario Gotze (kulia) baada ya kutua akitokea Borussia Dortmund majira ya joto
Mabingwa: Bayern imeanza kutetea ubingwa wa Ujerumani, Bundesliga kwa kushinda mechi mbili mfululizo
Inua glasi: Guardiola na benchi lake zima la ufundi watatumai kuendeleza wimbi la mafanikio msimu huu
Timu ya Bayern walifurajia na majagi na bia hizo mbili za Ujerumani, na kusherehekea kushinda taji Bundesliga-msimu uliopita kwa kumwagiana lita za bia Allianz Arena kabla ya kupokea taji la 23 la ubingwa wa Ujerumani.
Lakini kiungo Franck Ribery, ambaye ni muislamu safi, hakuwa mwenye furaha sana. Bahati nzuri kwake ni kwamba bia hiyo haikuwa na kilevi, na Mfaransa huyo alipigwa picha akiwa ameshika bia hiyo.
Mataji: Wachezaji wa Munich wakishereheeka na taji la Bundesliga baada ya kutwaa msimu uliopita
Chukua hiyo: Bastian Schweinsteiger akimwagiana na bia na mchezaji mwenzake, Daniel van Buyten
Franck Ribery akiogeshwa bia