IMEWEKWA AGOSTI 19, 2013 SAA 4: 19 ASUBUHI
MASHABIKI wenye hasira wa Arsenal wamemuandiki barua kali Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo Ivan Gazidis wakitaka kuona mabadiliko kwenye sera ya usajili ya timu hiyo baada ya vijana wa Arsene Wenger kuchapwa na Aston Villa kwa mabao 3-1 kwenye siku ya kwanza ya msimu.
MASHABIKI wenye hasira wa Arsenal wamemuandiki barua kali Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo Ivan Gazidis wakitaka kuona mabadiliko kwenye sera ya usajili ya timu hiyo baada ya vijana wa Arsene Wenger kuchapwa na Aston Villa kwa mabao 3-1 kwenye siku ya kwanza ya msimu.
Kichapo hicho cha Villa kimewatia hasira mashabiki wa klabu hiyo ambao wamechoshwa na mwelekeo wa klabu hiyo chini ya Stan Kroenke.
Arsenal wanafedha nyingi benki, wamelikuwa na faida kubwa na wanadau la pauni milioni 70 mkononi kwa ajili ya usajili, licha ya kelele zao zote wameshindwa kupambana na klabu tajiri za Ulaya kwenye soko la usajili.
VIDEO Nenda chini kaangalie Paul Lambert na Arsene Wenger wakizungumzia mchezo
Anakatisha tamaa: Mashabiki wa Arsenal wamemtumia barua kali Ivan Gazidis (juu) baada ya kuahidi usajili
Viongozi wa klabu hiyo wamedai kwamba wahukumiwe baada ya usajili kufungwa Septemba 2, mwaka huu, lakini Ligi Kuu England imeanza na usajili pekee wa Wenger ni kinda wa miaka 20, Yaya Sanogo bure kutoka Auxerre.
Sanogo alianzia benchi dhidi ya Villa wakati Christian Benteke, mshambuliaji ambaye aliomba kuhama Villa Park wakati huu wa kiangazi kabla ya kuamua kubaki akifunga mara mbili.
Arsenal wanaweza kujitetea kwamba maamuzi yaliwabana, lakini mechi ya Villa imeonyesha jinsi gani wana msimu mgumu mbele yao na kuzua mvutano kati ya wanaomuunga mkono Wenger na wale wanaotaka kuona mabadiliko.
Tumia fedha: Mashabiki wa Arsenal wanafikisha ujumbe kwa Wenger
Tumia fedha: Mashabiki wa Arsenal wanafikisha ujumbe kwa Wenger
Arsene: Defeat is a big disappointment
Splash the cash: Arsenal fans vent their anger at the Aston Villa game