IMEWEKWA AGOSTI 20, 2013 SAA 3:36 USIKU
BAADA ya kutua kwa mkopo Liverpool, Aly Cissokho amesema kwamba sasa ni wakati wa kupiga mzigo wa uhakika Anfield.
Beki huyo wa kushoto wa Valencia ametambulishwa na Wekundu hao na anatarajiwa kucheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Aston Villa Jumamosi.
Anakwenda kuchukua nafasi ya Jose Enrique katika safu ya ulinzi ya Anfield katika harakati za kocha Brendan Rodgers kusuka kikosi kamambe kitakachompa tiketi ya Ligi ya Mabingwa.
VIDEO Kaangalie video chini
Tayari kwa kazi: Aly Cissokho amesema yuko kuanza kazi Liverpool baada ya kutua akitokea Valencia kwa mkopo
Cissokho, ambaye atavaa jezi namba 20 alisema: "Najisikia furaha kwa kiasi kikubwa kuwa hapa na najivunia kazi ngumu niliyofanya hadi kufika hapa katika soka yangu.
"Wakati wote nimekuwa nikiota kusaini klabu gwiji. Nimekuwa mwenye bahati kiasi cha kutosha kuchezea klabu chache na kwa sasa kupata nafasi ya kuchezea klabu kama Liverpool, ni babu kubwa.
"Wakati wote nimesema, mbali na kuwapo wachezaji wengi wa Ufaransa, kwamba napenda haswa Ligi ya England, na pia nimekuwa na bahati kiasi cha kutosha kuchezea klabu fulani kubwa, katika fikra zangu nyuma, wakati wote nilitaka kucheza England.
Anasaini: Beki wa kushoto, Cissokho atavaa jezi namba 20 Anfield
Cissokho tayari amecheza Anfield, baada ya kuwamo katika kikosi cha Lyon kilichoshinda 2-1 katika hatua ya makundi kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2009.
Mazoezini: Cissokho (kulia kabisa) ameungana na wachezaji wenzake wapya Liverpool kukimbia Melwood
Ally Cissokho anatarajiwa kugombea namba na Jose Enrique katika beki ya kushoto
Wa mkopo: Cissokho amewasili Anfield kupiga kazi kwa muda akitokea Valencia
Makocha wa Liverpool wakimuangalia mchezaji mpya, Cissokho katika Uwanja wa mazoezi Melwood
Tabiri, nani yuko nyuma? Wachezaji wa Liverpool akiwemo Luis Suarez wakiwa na mchezaji mpya, Cissokho wakati wa mazoezi mepesi