• HABARI MPYA

    Saturday, August 24, 2013

    SHUGHULI ILIVYOKUWA PEVU SIMBA SC NA RHINO RANGERS ALLY HASSAN MWINYI LEO

    IMEWEKWA AGOSTI 24, 2013 SAA 4:00 USIKU
    Kiungo wa Simba SC, Jonas Mkude akishangilia baada ya kuifungia timu yake bao la kwanza katika mchezo wa leo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora dhidi ya wenyeji, Rhino Ranegrs. Timu hizo zilitoka 2-2.  

    Betram Mombeki aliwekewa ulinzi mkali leo

    Nahodha wa Simba SC, Nassor Masoud 'Chollo' akikabiliana na beki wa Rhino, huku kipa akijiandaa kuokoa 

    Kipa wa Rhino akidaka mbele ya Sino Augustino wa Simba SC 

    Mshambuliaji wa Rhino akimiliki mpira katikati ya wachezaji wa Simba SC

    Haroun Chanono akipasua katikati ya wachezaji wa Rhino

    Nurdin Bakari wa Rhino akikabiliana na Haroun Chanono

    Betram Mombeki akipambana katika kona

    Yule anaugulia maumivu, wengine wanagaagaa chini. Hivi ndivyo ilivyokuwa Mwinyi leo

    Haroun Chanono anawatoka wachezaji wa Rhino

    Refa anampa kadi ya njano Mombeki

    Abbel Dhaira kama hahusiki vile...Ni baada ya Rhino kufunga bao la kwanza. Nurdin Bakari anaokota mpira nyavuni wakasake mabao zaidi

    Kitu nyavuni, kipa wa Rhino akiruka bila mafanikio baada ya mkwaju wa penalti wa Jonas Mkude

    Shangwe za bao, Jonas Mkude akishangilia bao lake la pili leo 

    Wachezaji wa Rhino wakishangilia bao la kusawazisha

    Miraj Adam akipambana na mshambuliaji wa Rhino

    Said Ndemla akifungishwa tela na mchezaji wa Rhino

    Benchi la Simba SC baada ya Rhino kuchomoa 

    Makocha...King Kibaden na Jamhuri Kihwelo 'Julio' 

    Mashabiki wa Rhino wakiitia moto jezi ya Simba SC

    Hadi huruma; Shabiki wa Simba aliyetoka Dar es Salaam kuja kuisapoti timu yake akiwa hoi baada ya sare

    Vijana wa kazi; Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), wamiliki wa Rhino akiwa juu ya gari lao wakitazama mpira

    Hawa ndiyo Rhino, timu nzuri na wachezaji wazuri

    Wekundu wa Msimbazi, Simba SC ya leo

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: SHUGHULI ILIVYOKUWA PEVU SIMBA SC NA RHINO RANGERS ALLY HASSAN MWINYI LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top