IMEWEKWA AGOSTI 24, 2013 SAA 7:40 MCHANA
KLABU ya Arsenal imefufua mpango wa kumsajili Emiliano Viviano katika msako wa kipa.
Kocha Arsene Wenger anaendelea kusaka mshambuliaji mwenye jina na kiungo mkabaji, lakini wasaka vipaji wa klabu hiyo nao watamuangalia kipa wa Espanyol, Kiko Casilla leo akicheza dhidi ya Valencia.
Pamoja na kufuatiliwa na Arsenal, kocha wa Espanyol, Javier Aguirre tayari amesema anataka kumbakiza Casilla, mwenye umri wa miaka 26, akisema: "Casilla hawezi kuondoka, si hiyo. Namuona anayejihusisha sana na naamini hataondoka,".
Mlengwa: Kipa Emiliano Viviano anaweza kuhamia London
Arsenal pia inamfuatilia Vincent Guaita wa Valencia, lakini hatarajiwi kucheza leo.
Kipa wa Italia, Viviano, yupo pia baada ya klabu yake, Palermo kushuka na imeamua kumuuza.
Msimu uliopita alicheza kwa mkopo Fiorentina lakini hawaamua zaidi, wakati kuna suala la mmiliki wa tatu linalohitaji pia kutatuliwa.
Arsenal imekuwa ikimfuatilia Viviano kwa miaka mitatu iliyopita, lakini imekuwa ikitajiwa bei kubwa na kushindwa kumnunua.
Na huyu: Kipa wa Espanyol, Kiko Casilla pia yumo kwenye rada za Arsene Wenger
Wakati huo huo, Schalke inamtaka Lukas Podolski kwa mkopo jambo ambalo Arsenal hawawezi kukubali hadi labda wapate mshambuliaji mwingine mkali.
Arsenal pia inammezea mate beki wa kulia wa Schalke, Atsuto Uchida lakini Wajerumani hawako tayari kumuuza.
Schalke, pia inamtaka mshambuliaji wa Chelsea, Demba Ba kama ilivyo kwa Hoffenheim.