IMEWEKWA AGOSTI 30, 2013 SAA 10: 57 JIONI
MSHAMBULIAJI Samuel Eto'o amesainisi Mkataba wa mwaka mmoja na Chelsea jana kwa mshahara wa Pauni Milioni 7 kwa mwaka.
Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 32 ametambulishwa rasmi leo baada ya kukamilisha vipimo vya afya.
Mwanasoka huyo bora mara nne Afrika ambaye aliwasili London juzi usiku kwa treni kutoka Ufaransa hadi Stesheni ya St. Pancras, alisema: "Nimeona ubora ambao wanao Chelsea, na nimekuwa nikimfurahia sana Jose Mourinho kabla, hivyo wakati nafasi inapotokea, huwa nafurahia kuichukua.
Uzi wa bluu: Eto'o akiwa na jezi ya Chelsea
Anamwaa wino: Eto'o akisaini Mkataba na Katibu wa Chelsea, David Barnard
Raha kuwa hapa: Eto'o amesaini kama mchezaji huru