IMEWEKWA AGOSTI 26, 2013 5:58 USIKU
KOCHA wa Manchester United, David Moyes amepeleka ujumbe kwa Chelsea kwamba Wayne Rooney hatahamia Stamford Bridge majira haya ya joto kufuatia mchezo wa usiku huu wa miamba hao uliomalizika kwa sare ya bila kufungana kwenye Uwanja wa Old Trafford.
Rooney alianza katika kikosi cha kwanza baada ya tetesi za muda mrefu majira haya ya joto kwamba atajiunga na Jose Mourinho Magharibi mwa London, lakini alipiga soka ya uhakika leo akiwa na uzi mwekundu.
Rooney akimdhibiti Ramires |
Katika mchezo huo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Enlgand baina ya timu hizo, United ilianzisha washambuliaji watatu, Welebeck, Rooney na Van Persie.
Dakika ya 65 Lampard alishika kabisa mpira kwenye eneo la hatari kufuatia shuti la Cleverley, lakini refa 'akapeta'.
Dakika ya 71 Ashely Cole alianguka kwenye eneo la hatari wakati akikabiliana na Jones na akalilia penalti na hata Mournho akaonekana kulalamika akiwa kwenye benchi.
Mchezo ulikuwa mkali na timu hizo zilishambuliana kwa zamu na baada ya mechi wachezaji walipongezana kwa mchezo mzuri.
Jose Mourinho alisema baada ya mechi mchezo ulikuwa wa haki na hadhani kama kuna iliyomzidi mwenzake uwezo, wakati Moyes alilalamikia penalti ya Lampard kuunawa mpira na kuwapongeza vijana wake kwa soka nzuri.
Kikosi cha Man United kilikuwa: De Gea, Jones, Ferdinand, Vidic, Evra, Valencia/Young dk67, Cleverley, Carrick, Welbeck/Giggs dk78, Rooney na Van Persie.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Cahill, Terry, Cole, Ramires, Lampard, De Bruyne/Torres dk60, Oscar, Hazard/Azpilicueta dk93 na Schurrle.
Amerudi kikosi cha kwanza: Rooney alianza katika kikosi cha kwanza na alicheza vizuri akipiga mashuti mazuri mawili yaliyokaribia kuzaa mabao Old Trafford
Rafu: Cole akimchezea rafu RVP
Cole akimdhibiti RVP
Mpira wa mikono? Lampard akiwa ameshika mpira kwa mikono ndani ya eneo la hatari na refa hakutoa penalti, ingawa anashuhudia tukio hapo
Kipa? Lampard alibeba majukumu ya kipa wake dakika ya 65
Alijirusha? Cole alianguka kwenye eneo la hatari na kulilia penalti, wakati akikabiliana na Jones
Analilia penalti: Kocha Jose Mourinho akilalamika baada ya Cole kuanguka na refa hakutoa penalti
Zama mpya, kocha mpya: Moyes akiiongoza United leo baada ya kurithi mikoba ya Sir Alex Ferguson mwishoni mwa msimu
Mapokezi mazuri; Moyes akisaini karatasi za mashabiki
Rooney anatakiwa na Chelsea, lakini leo alipandishwa kikosi cha kwanza
Cole akikabiliana na Rooney
Mourihno na Moyes wakisalimiana kabla ya mechi Old Trafford