IMEWEKWA AGOSTI 17, 2013 SAA 9:38 ALASIRI
KOCHA wa Barcelona, Tata Martino amepuuza taarifa za mpango wa kuwasajili David Luiz au Daniel Agger, kwa kuthibitisha anafuarahia safu ya sasa ya ulinzi.
Vigogo hao wa Katalunya wamekuwa wakihusishwa kutaka kuwasajili kwa fedha nyingi wachezaji hao wa klabu za Ligi Kuu England, Chelsea na Liverpool.
Na kocha huyo mpya amesema katika Mkutano na Waandishi wa Habari kuelekea mchezo wake wa kwanza wa La Liga dhidi ya Levante: "Tuna Puyol, Pique, Mascherano, Bartra, pia Adriano. Ikiwa kuna majeruhi yeyote, usajili wa Januari utakuja miezi michache ijayo,".
VIDEO Kaangalia Martino akirithi mikoba ya Vilanova Barcelona
Hahitajiki: Barcelona ilifikiriwa kutaka kusajili beki wa kati majira haya ya joto na David Luiz (juu) na Daniel Agger walitajwa kuwamo kwenye orodha ya wanaotakiwa
Klabu hiyo ya Hispania ilisumbuliwa na tatizo la majeruhi msimu uliopita, iliyowaponza kuchapwa 7-0 katika Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa na Bayern Munich.
Lakini kauli ya kocha mpya inamaanisha makocha wenzake, Brendan Rodgers na Jose Mourinho wanaweza kutuliza presha zao.
Rodgers amempa Agger Unahodha Msaidizi katika kumshawishi abaki Anfield, wakati Mourinho alisema kuhusu Luiz: "Tunataka kumbakiza na tunafahamu kwamba klabu kubwa kama Barcelona wanataka kilicho bora na wanajaribu kupata moja kati ya mabeki bora wa kati duniani, lakini tumekuwa wazi sana kwa kusema kwamba hakuna nafasi ya David Luiz kuondoka,".
Mambo hadharani: Tata Martino akizungumza na Waandishi wa Habari kuelekea mchezo wake wa kwanza wa mashindano tangu aanze kazi Barca