IMEWEKWA AGOSTI 17, 2013 SAA 3:21 USIKU
KOCHA Arsene Wenger ameanza vibaya Ligi Kuu ya England baada ya kuchapwa mabao 3-1 na Aston Villa Uwanja wa Emirates leo.
Kocha huyo Mfaransa amesaini mchezaji mmoja tu ambaye pia ni majeruhi baada ya kutemwa wachezaji 17.
Wachezaji wawili wa Arsenal, Keiron Gibbs na Alex Oxlade-Chamberlain walilazimika kutoka nje kipindi cha kwanza baada ya kuumia na Christian Benteke alikuwa kinara wa ushindi wa Villa.
Benteke alifunga mabao mawili katika dakika za 21na 60 wakati bao lingine lilifungwa na Luna dakika ya 84, wakati Arsenal ilitangulia kupata bao dakika ya tano kupitia kwa Olivier Girous.
Kikosi cha Arsenal kilikuwa: Szczesny, Sagna/Podolski dk90, Koscielny, Mertesacker, Gibbs/Jenkinson dk5, Wilshere, Ramsey, Rosicky, Walcott, Chamberlain/Cazorla dk5 na Giroud
Villa: Guzan, Lowton, Vlaar, Baker/Clark dk7, Luna, El Hamadi, Westwood, Delph, Agbonlahor, Weimann/Bacuna dk88 na Benteke,
VIDEO Kaangalia chini Paul Lambert: Agbonlahor na Benteke
Mshambuliaji wa Arsenal, Olivier Giroud akifunga bao la kuongoza
Takwimu za mechi ya Arsenal na Aston Villa
Giroud akishangilia
Ameokoa: Kipa wa Arsenal, Wojciech Szczesny akipangua mkwaju wa penalti wa Benteke...
...lakini Benteke akafunga baada ya kuuwahi mpira uliorudi
Damu: Mchezaji wa Arsenal, Kieran Gibbs akiigulia maumivu chini baada ya kugongana na Andreas Weimann wa Villa
Gibbs akitolewa baada ya kuumia kichwa
Mchezaji wa Villa, Ron Vlaar, wa pili kulia akiokoa
Mchezaji wa Arsenal, Tomas Rosicky, chini akipambana na Karim El Ahmadi wa Villa
Utata: Santi Cazorla, Per Mertesacker na Wojciech Szczesny wakiwa hawaamini refa Anthony Taylor amewapa Villa penalti ya pili
Shabiki wa Arsenal akipeleka wa wazi kwa Wenger kumtaka asajili
Mwanzo mbaya: Wenger akisikitika baada ya kipigo
Katika mchezo mwingine, bao pekee la Daniel Sturridge dakika ya 37, lilitosha kuipa Liverpool ushindi wa 1-0 nyumbani dhidi ya Stoke City.
Kikosi cha Liverpool kilikuwa: Mignolet, Johnson, Toure, Agger, Enrique, Lucas, Henderson, Gerrard, Coutinho, Sturridge, Aspas/Sterling dk71.
Stoke: Begovic, Cameron, Huth, Shawcross, Pieters, N'Zonzi, Whelan/Adam dk62, Wilson, Etherington/Pennant dk62, Walters na Crouch/Jones dk81.
Suarez mpya? Sturridge akifunga