• HABARI MPYA

    Monday, March 04, 2024

    FODEN APIGA MBILI MAN CITY YAICHAPA UNITED 3-1


    MABINGWA watetezi, Manchester City wamewadhibu mahasimu, Manchester United kwa kuwatandika mabao 3-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Uwanja wa Etihad Jijini Manchester.
    Ni Manchester United waliotangulia kwa bao la Marcus Rashford dakika ya nane, kabla ya Manchester City kutoka nyuma kwa mabao ya Philip Foden dakika ya 56 na 80 na Erling Haaland dakika ya 90+1.
    Kwa ushindi huo, Manchester City wanafikisha pointi 62, ingawa wanabaki nafasi ya pili wakizidiwa pointi moja na Liverpool baada ya wote kucheza mechi 27, wakati Manchester United wanabaki na pointi zao 44 za mechi 27 pia nafasi ya sita.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: FODEN APIGA MBILI MAN CITY YAICHAPA UNITED 3-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top