• HABARI MPYA

    Thursday, February 29, 2024

    PRISONS YAKWEA TANO BORA LIGI KUU BAADA YA KUICHAPA TABORA UNITED 2-1

    TIMU ya Tanzania Prisons jana iliibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Tabora United katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
    Mabao ya Tanzania Prisons yalifungwa na Zabona Mayombya dakika ya 21 na Samson Mbangula dakika ya 88, huku bao pekee la Tabora United likifungwa na Erick Okutu dakika ya 17.
    Kwa matokeo hayo, Tanzania Prisons inafikisha pointi 24 na kusogea nafasi ya tano, wakati Tabora United inabaki na pointi zake 18 nayo inabaki nafasi ya 13 baada ya wote kucheza mechi 18.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PRISONS YAKWEA TANO BORA LIGI KUU BAADA YA KUICHAPA TABORA UNITED 2-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top