WENYEJI, Tabora United wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara mchana wa leo Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora.
Mshambuliaji hatari raia wa Ghana, Eric Okutu alianza kuifungia Tabora United dakika ya 11, kabla ya kiungo mzawa, Pius Buswita kuisawazishia Namungo FC dakika ya 37.
Kwa matokeo hayo, Namungo FC wanafikisha pointi 18 na kusogea nafasi ya saba na Tabora United wanatimiza pointi 16, ingawa wanabaki nafasi ya 12 baada ya wote kucheza mechi 15.
0 comments:
Post a Comment