TIMU ya JKT Tanzania imelazimishwa sare ya bila mabao na Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Meja Jenerali Mstaafu Isamuhyo, Mbweni Jijini Dar es Salaam.
Kwa matokeo hayo, JKT Tanzania inafikisha pointi 17 na kusogea nafasi ya 11, wakati Namungo FC imetimiza pointi 19 na kupanda nafasi ya nane baada ya wote kucheza mechi 16.
0 comments:
Post a Comment