• HABARI MPYA

    Tuesday, February 20, 2024

    TIMU ZA LIGI KUU ZAZICHUJA ZA CHAMPIONSHIP KWENYE ASFC


    TIMU za Coastal Union, Singida Fountain Gate na Dodoma Jiji zimelinda hadhi ya Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya kuzitoa timu za NBC Championship katika Hatua ya 32 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC).
    Coastal Union iliichapa Mbeya Kwanza 1-0 Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga, Singida Fountain Gate ikaichapa 2-0 Fountain Gate Talents Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza na Dodoma Jiji ikailaza 2-1 Biashara United Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
    Michuano ya ASFC Hatua ya 32 Bora inaendelea leo kwa mabingwa watetezi, Yanga kumenyana na Polisi Tanzania kuanzia Saa 1:00 usiku Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
    FEBRARI 20, 2024
    Mashujaa FC         v Mkwajuni
    KMC v Gunners FC
    Yanga SC v Polisi Tanzania
    Kagera Sugar         v Pamba FC
    FEBRUARI 21, 2024
    Mtibwa Sugar         v Stand nited
    Namungo FC         v Transit Camp
    FEBRUARI 22, 2024
    Tabora United         v Nyamongo SC
    Azam FC v Green Warriors
    Ihefu SC         v Mbuni FC
    JKT Tanzania         v TMA Stars
    Geita Gold         v Mbeya City
    FEBRUARI 27, 2024
    Simba SC v TRA Kilimanjaro

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TIMU ZA LIGI KUU ZAZICHUJA ZA CHAMPIONSHIP KWENYE ASFC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top