TUZO ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu mwezi Januari imekwenda kwa kiungo Mbrazil wa Singida Big Stars, Bruno Gomez akiwapiku Ibrahim Abdallah Mkoko wa Namungo FC na mshambuliaji Mkongo, Henock Mayala wa Polisi Tanzania.
Aidha, kocha Mholanzi wa Singida Big Stars, Hans van der Pluijm amebeba tuzo ya Kocha Bora akwapiku Mbrazil, Robert Oliviera wa Simba na Mtunisia, Nasredine Nabi wa Yanga.
0 comments:
Post a Comment