RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan ameahidi kuichangia timu ya taifa ya wanawake, Twiga Stars kiasi Sh. Milioni 15.
Rais Samia alitoa ahadi hiyo wakati akizungumza kwa simu na Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba kwenye tamasha la harambee ya kuchangia Twiga Stars lililopewa jina, Orange Concect.
Kwa upande wake, Waziri Nchemba ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kutoa udhamini kwenye timu za wanawake ili ziweze kuendelea kufanya vizuri.
Nchemba amesema Mheshimiwa Rais amefanya mambo makubwa siyo tu kwenye sekta ya Michezo bali katika sekta mbalimbali.
0 comments:
Post a Comment