MABAO ya mshambuliaji wa Manchester United, Bruno Fernandes dakika ya 32 na 65 jana yaliipa Ureno ushindi wa 2-0 dhidi ya Macedonia Kaskazini katika mchezo wa mwisho wa mchujo wa kuwania tiketi ya Fainali za Kombe la Dunia Uwanja wa Do Dragão Jijini Porto.
Macedonia Kaskazini iliyoitoa Italia katika mechi ya kwanza ya mchujo, ilishindwa kufurukuta mbele ya Ureno iliyoongozwa na gwiji wake, mshambuliaji wa Manchester United.
0 comments:
Post a Comment