• HABARI MPYA

    Saturday, March 12, 2022

    RUVU YAITANDIKA COASTAL 3-1 MKWAKWANI

    WENYEJI, Coastal Union wamechapwa mabao 3-1 na Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
    Mabao ya Ruvu Shooting leo yamefungwa na Pius Buswita dakika ya 19, Haroun Chanongo dakika ya 31 na Samson Joseph dakika ya 79, wakati la Coastal limefungwa na Vincent Abubakar dakika ya 22.
    Kwa ushindi huo, Ruvu Shooting inafikisha pointi 20 na kusogea nafasi ya 11, ikizidiwa pointi moja na Coastal baada ya wote kucheza mechi 18.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RUVU YAITANDIKA COASTAL 3-1 MKWAKWANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top