BAO la Bukayo Saka dakika ya 30 limeipa Arsenal ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Aston Villa katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Jumamosi Uwanja wa Villa Park Jijini Birmingham.
Kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 54 na kuendelea kukaa nafasi ya nne, ikizidiwa tano na Chelsea baada ya wote kucheza mechi 28, wakati Aston Villa inabaki na pointi zake 36 za mechi 29 nafasi ya tisa.
0 comments:
Post a Comment