WENYEJI, Azam FC wameibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 23 ya Somalia katika mchezo wa kirafiki jioni ya leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Mabao ya Azam FC yamefungwa na Ayoub Lyanga dakika ya 64, Idris Mbombo dakika ya 81 na Shaaban Iddi Chilunda dakika ya 90 na ushei.
Somalia U23 katika mchezo wao wa kwanza wa kirafiki walitoka sare ya 1-1 na vigogo, Yanga hapo hapo Azam Complex.
0 comments:
Post a Comment