WENYEJI, Mtibwa Sugar wameibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Geita Gold katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Manungu Complex, Turiani mkoani Morogoro.
Mabao ya Mtibwa Sugar yamefungwa na Nzigamasabo Steve dakika ya 27 na Mululi Mayanja dakika ya 76 na kwa ushindi huo wanafikisha pointi 19 na kusogea nafasi ya 12, wakati Geita Gold inabaki na pointi zake 21 katika nafasi ya tisa baada ya wote kucheza mechi 18.
0 comments:
Post a Comment