• HABARI MPYA

    Monday, March 28, 2022

    AZAM FC KUMENYANA NA DTB JUMANNE




    TIMU ya Azam FC itakuwa na mechi ya kirafiki dhidi ya DTB Jumanne Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. 
    Kwa Azam, mechi hiyo ni sehemu ya maandalizi ya mchezo wao ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Yanga SC Aprili 6, mwaka huu hapo hapo Azam Complex.
    Na kwa DTB mechi hiyo ni ya kujipanga kwa michezo yake ijayo ya ligi ya kuwania kupanda Ligi Kuu, ijulikanayo kama Championship.
    Ikumbukwe Yanga wao watakuwa na mechi ya kujipima pia Jumatano hapo hapo Chamazi dhidi ya Mafunzo ya Zanzibar.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC KUMENYANA NA DTB JUMANNE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top