WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa ameitembelea timu ya taifa ya wasichana chini ya umri wa miaka 17 iliyoweka kambi visiwani Zanzibar kujiandaa na mchezo wa marudiano kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Botswana Machi 20, 2022.
Mabinti wa Tanzania U17 walishinda 7-0 kwenye mchezo wa kwanza wiki iliyopita na wakivuka hatua hii watakutana na Burundi katika Raundi ya Tatu kuwania kwenda Raundi ya mwisho ya mchujo.
0 comments:
Post a Comment