• HABARI MPYA

    Friday, March 11, 2022

    WAZIRI WA MICHEZO AWATEMBELEA WASICHANA U17


    WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa ameitembelea timu ya taifa ya wasichana chini ya umri wa miaka 17  iliyoweka kambi visiwani Zanzibar kujiandaa na mchezo wa marudiano kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Botswana Machi 20, 2022.
    Mabinti wa Tanzania U17 walishinda 7-0 kwenye mchezo wa kwanza wiki iliyopita na wakivuka hatua hii watakutana na Burundi katika Raundi ya Tatu kuwania kwenda Raundi ya mwisho ya mchujo.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WAZIRI WA MICHEZO AWATEMBELEA WASICHANA U17 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top