• HABARI MPYA

    Friday, September 10, 2021

    PRINCE DUBE AFANYIWA UPASUAJI

    MSHAMBULIAJI Mzimbabwe wa Azam FC,  Prince Dube Mpumelelo amefanyiwa upasuaji utakaomuweka nje kwa wiki sita.
    Taarifa ya Azam FC imesema kwamba upasuaji huo uliofanikiwa umefanyika katika hospitali ya Vincent Pellotti jijini Cape Town Afrika Kusini.
    "Hali yake ni nzuri na panapo majaaliwa kesho atatolewa hospitali na Jumatatu atawasilia Dar es Salaam kuendelea kujiuguza," amesema Thabit Zakaria 'Zaka Zakazi' katika taarifa yake kwa vyombo vya Habari.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PRINCE DUBE AFANYIWA UPASUAJI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top