• HABARI MPYA

    Sunday, July 29, 2018

    WHYTE AMSHINDA PARKER KWA POINTI NA KUTWAA TAJI LA WBC

    Bondia Dillian Whyte akimtazama mpinzani wake, Joseph Parker baada ya kumuangusha chini kwa mara ya pili katika raundi ya tisa alipomchapa ngumi kali ya kushoto katika pambano la raundi 12 kuwania mkanda wa WBC uzito wa Silver Heavy ukumbi wa 02 Arena mjini London. Whyte alishinda kwa pointi za majaji wote ( 115-110, 114-111, 113-112) na kutwaa taji hilo la WBC lililokuwa wazi na kujiweka kwenye mazingira mazuri ya kuwania mkanda wa dunia, kwa uwezekano wa kurudiana na Muingereza mwenzake, Anthony Joshua baada ya kupoteza pambano la kwanza Desemba 12 mwaka 2015 kwa TKO raundi ya saba 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WHYTE AMSHINDA PARKER KWA POINTI NA KUTWAA TAJI LA WBC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top