BARCELONA imeendelea kuitumulia vumbi Real Madrid katika mbio za taji la La Liga, baada ya jioni ya leo kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Valencia Uwanja wa Camp Nou.
Luis Suarez aliifungia Barcelona dakika ya kwanza, kabla ya Claudio Bravo kupangua penalti Nahodha wa Valencia, Dani Parejo dakika ya tisa.
Lionel Messi akaihakikishia Barca pointi tatu dakika ya 90, ambalo linakuwa bao lake 400 tangu aanze kuichezea Barcelona.
Barca sasa inatimiza pointi 78 baada ya kucheza mechi 32, ikifuatiwa na Real yenye pointi 73 za mechi 31. Real inamenyana na Malaga baadaye usiku huu.
Lionel Messi (kushoto), Luis Suarez (katikati) na Neymar wakishangilia bao la Suarez dhidi ya Valencia leo
0 comments:
Post a Comment