Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
KIKOSI cha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kimeondoka alfajiri ya leo kwenda Afrika Kusini kuweka kambi ya siku mbili kabla ya kwenda Swziland Novemba 13, mwaka huu.
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij ameondoka na wachezaji 24 kwa ajili ya mechi ya kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) dhidi ya Swaziland itakayochezwa Novemba 16, mwaka huu mjini Mbabane.
Kikosi hicho kiliingia kambini Saa 6:00 mchana wa jana kwenye hoteli ya Accomondia, kabla ya jioni yake kufanya mazoezi kwenye gym.
Wachezaji walioitwa kwenye kikosi hicho ni makipa Aishi Manula (Azam) na Deogratias Munishi (Yanga). Mabeki ni Abubakar Mtiro (Kagera Sugar), Aggrey Morris (Azam), Emmanuel Simwanda (African Lyon), Hassan Isihaka (Simba), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Osacr Joshua (Yanga), Said Moradi (Azam), Salim Mbonde (Mtibwa Sugar) na Shomari Kapombe (Azam).
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Haruna Chanongo (Simba), Himid Mao (Azam), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Said Ndemla (Simba) na Salum Abubakar (Azam).
Washambuliaji ni Juma Luizio (ZESCO, Zambia), Mbwana Samata (TP Mazembe, DR Congo), Mrisho Ngasa (Yanga), Simon Msuva (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DR Congo).
Mara ya mwisho, Stars iliifunga 4-1 Benin katika mchezo wa kirafiki unaotambuliwa na FIFA pia, Oktoba 12, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
KIKOSI cha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kimeondoka alfajiri ya leo kwenda Afrika Kusini kuweka kambi ya siku mbili kabla ya kwenda Swziland Novemba 13, mwaka huu.
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij ameondoka na wachezaji 24 kwa ajili ya mechi ya kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) dhidi ya Swaziland itakayochezwa Novemba 16, mwaka huu mjini Mbabane.
Kikosi hicho kiliingia kambini Saa 6:00 mchana wa jana kwenye hoteli ya Accomondia, kabla ya jioni yake kufanya mazoezi kwenye gym.
![]() |
Amri Kiemba yumo kwenye kikosi cha Taifa Stars kilichokwenda Afrika Kusini |
Wachezaji walioitwa kwenye kikosi hicho ni makipa Aishi Manula (Azam) na Deogratias Munishi (Yanga). Mabeki ni Abubakar Mtiro (Kagera Sugar), Aggrey Morris (Azam), Emmanuel Simwanda (African Lyon), Hassan Isihaka (Simba), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Osacr Joshua (Yanga), Said Moradi (Azam), Salim Mbonde (Mtibwa Sugar) na Shomari Kapombe (Azam).
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Haruna Chanongo (Simba), Himid Mao (Azam), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Said Ndemla (Simba) na Salum Abubakar (Azam).
Washambuliaji ni Juma Luizio (ZESCO, Zambia), Mbwana Samata (TP Mazembe, DR Congo), Mrisho Ngasa (Yanga), Simon Msuva (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DR Congo).
Mara ya mwisho, Stars iliifunga 4-1 Benin katika mchezo wa kirafiki unaotambuliwa na FIFA pia, Oktoba 12, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment