• HABARI MPYA

    Thursday, November 27, 2014

    RONALDO AING'ARISHA REAL MADRID LIGI YA MABINGWA ULAYA

    BAO pekee la Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo limeipa ushindi wa 1-0 ugenini Real Madrid dhidi ya FC Basle katika mchezo wa Kundi B Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu.
    Mreno huyo, aliyeondoka Manchester United kutua Madrid kwa dau la rekodi, alifunga bao hilo pekee muhimu dakika ya 35 akimalizia kazi nzuri ya Mfaranda, Karim Benzema.
    Real Madrid sasa inaongoza Kundi B kwa rekodi nzuri ya ushindi, huku ikiwa imesaliwa na mecni moja, wakati kwa kipigo cha leo, Basle hatima yao itajulikana baada ya mechi ya mwisho dhidi ya Liverpool kama watasonga mbele au, la.
    Kikosi cha Basle kilikuwa; Vaclik, Degen/Hamoudi dk76, Schar, Suchy, Safari, Elneny, Frei/Diaz dk83, Zuffi/Kakitani dk87, Gonzalez, Embolo na Gashi.
    Real Madrid: Navas, Arbeloa, Varane, Ramos, Coentrao, Kroos, Isco/Nacho dk93, Rodriguez/Marcelo dk89, Bale, Ronaldo na Benzema/Illarramendi dk71.
    Cristiano Ronaldo celebrates the opening goal for Real Madrid after taking advantage of an excellent run by Karim Benzema
    Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kuifungia bao pekee Real Madrid 
    Gareth Bale wa Real Madrid akipambana na beki wa Basle, Philipp Degen 

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2850941/Basle-0-1-Real-Madrid-Cristiano-Ronaldo-bundles-home-Lionel-Messi-toes.html#ixzz3KDcQmJLf 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO AING'ARISHA REAL MADRID LIGI YA MABINGWA ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top