// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); PAZIA LA KUFUZU AFCON 2015 LAFUNGWA JANA, DRC WAPENYA ‘KIPANYA PANYA’ - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE PAZIA LA KUFUZU AFCON 2015 LAFUNGWA JANA, DRC WAPENYA ‘KIPANYA PANYA’ - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, November 20, 2014

    PAZIA LA KUFUZU AFCON 2015 LAFUNGWA JANA, DRC WAPENYA ‘KIPANYA PANYA’

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    MECHI za kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani Equatorial Guinea zimefikia tamati jana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imefuzu kama mshindi wa tatu bora.
    Kongo imekamilisha nafasi ya mwisho katika siti za ndege za kwenda Equatorial Guinea 2015 baada ya kuwa timu iliyomaliza nafasi ya tatu ikiwa na wastani mzuri zaidi wa matokeo kutoka makudi yote saba.
    Mabingwa hao wa mwaka 1968 na 1974, walipata nafasi hiyo baada ya Misri kufungwa mabao 2-1 na wapinzani wao wa Kaskazini mwa Afrika, Tunisia katika Kundi G mjini Monastir.
    DRC wamefuzu kama washindi wa tatu wa bora, wakiipiku Misri

    DRC ambayo iliifunga Sierra Leone 3-1 mjini Kinshasa, imemaliza na pointi tisa, ambazo ni nyingi zaidi kwa timu zilizomaliza nafasi ya tatu kwenye makundi yote saba.
    Mabingwa mara saba, Misri, wameshindwa kufuzu kwa mara ya tatu mfululizo baada ya Tunisia kutoka nyuma na kuwafunga. Mafarao, waliongoza hadi mapumziko kwa bao la mshambuliaji wa Chelsea, Mohamed Salah kabla ya Tunisia kuzinduka na kupata mabao kupitia kwa Yassine Chikaoui dakika ya 52 na Whabi Khazri dakika tisa kabla ya filimbi ya mwisho.
    Nchi zilizofuzu AFCON ya mwakani mbali ya wenyeji Equatorial Guinea; ni Algeria, Burkina Faso, Cape Verde, Cameroon, Kongo, Ivory Coast, DRC, Gabon, Ghana, Guinea, Mali, Senegal, Afrika Kusini, Tunisia na Zambia.
    Saydou Keita ameiongoza Mali kufuzu jana
    MSIMAMO WA MAKUNDI BAADA YA MECHI ZA KUFUZU AFCON 2015
    Kundi A
    Timu  P W D L GF GA GD Pts
    1 A. Kusini 6 3 3 0 9 3 6 12
    2 Congo 6 3 1 2 6 6 0 10
    3 Nigeria 6 2 2 2 9 7 2 8
    4 Sudan 6 1 0 5 3 11 -8 3

    Kundi B
    Timu  P W D L GF GA GD Pts
    1 Algeria 6 5 0 1 11 4 7 15
    2 Mali 6 3 0 3 8 6 2 9
    3 Malawi 6 2 1 3 5 9 -4 7
    4 Ethiopia 6 1 1 4 7 12 -5 4

    Kundi C
    Timu  P W D L GF GA GD Pts
    1 Gabon 6 3 3 0 9 4 5 12
    2 Burkina Faso 6 3 2 1 8 4 4 11
    3 Angola 6 1 3 2 5 5 0 6
    4 Lesotho 6 0 2 4 3 12 -9 2
    Group D

    Timu  P W D L GF GA GD Pts
    1 Cameroon 6 4 2 0 9 1 8 14
    2 Ivory Coast 6 3 1 2 13 11 2 10
    3 DRC          6 3 0 3 10 9 1 9
    4 Sierra Leone 6 0 1 5 3 14 -11 1

    Kundi E
    Timu  P W D L GF GA GD Pts
    1 Ghana 6 3 2 1 11 7 4 11
    2 Guinea 6 3 1 2 10 8 2 10
    3 Uganda 6 2 1 3 4 5 -1 7
    4 Togo        6 2 0 4 7 12 -5 6

    Kundi F
    Timu  P W D L GF GA GD Pts
    1 Cape Verde  6 4 0 2 9 6 3 12
    2 Zambia 6 3 2 1 6 2 4 11
    3 Msumbiji  6 1 3 2 4 4 0 6
    4 Niger 6 0 3 3 4 11 -7 3

    Kundi G
    Timu  P W D L GF GA GD Pts
    1 Tunisia 6 4 2 0 6 2 4 14
    2 Senegal 6 4 1 1 8 1 7 13
    3 Misri  6 2 0 4 5 6 -1 6
    4 Botswana 6 0 1 5 1 11 -10 1
    Ivory Coast imefuzu pia Fainali za Mataifa ya Afrika
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PAZIA LA KUFUZU AFCON 2015 LAFUNGWA JANA, DRC WAPENYA ‘KIPANYA PANYA’ Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top