Na Emanuel Madafa, MBEYA
SIKU chache baada ya kocha, Juma Mwambusi kutangaza kujiuzulu, kumeibuka tetesi kwamba huenda kocha huyo akarejea kukinoa kikosi hicho endapo uongozi utaridhia baadhi ya masharti aliyoyapendekeza kocha huyo.
Habari za ndani zilizotufikia zinasema kwamba uongozi wa klabu hiyo, umeonyesha imani kubwa na kocha Mwambusi hivyo kumtaka kurejea tena kikosini.
Moja ya masharti ambayo yamewekwa bayana na kocha huyo kwamba ni lazima uongozi kuyatekeleza ni kwamba endapo atarejea kikosini asingependa uongozi kumuingilia kwenye majukumu yake ya kiutendaji.
Pia uongozi, huo umetakiwa kuweka mipaka kwa mashabiki ambao kwa sasa wameonekana kuitawala klabu hiyo hadi kufikia hatua ya kuingilia utendaji wa mwalimu kwa kumtaka kupanga wachezaji wanaowataka wao.
Akizungumzia hilo, Meya wa Jiji la Mbeya, Athanas Kapunga ambaye pia ni mwenyekiti wa bodi ya timu hiyo, amesema suala la kocha kujiuzulu bado linafanyiwa kazi na uongozi na kwamba vikao vya kulijadili bado vinaendelea kufanyika.
Amesema bado wanaendelea na vikao vya ndani hivyo suala la kocha Mwambusi liko mezani nakwamba hivi sasa ndio wanaelekea kulijadili na kulitolea tamko kesho Nov 21 katika mara baada ya kukamilika kwa baraza la Madiwani.
Hata hivyo masharti ya kocha huyo yametajwa kuwa huenda yakawagharimu baadhi ya viongozi. Imehamishwa kutoka http://www.jamiimoja.blogspot.com
SIKU chache baada ya kocha, Juma Mwambusi kutangaza kujiuzulu, kumeibuka tetesi kwamba huenda kocha huyo akarejea kukinoa kikosi hicho endapo uongozi utaridhia baadhi ya masharti aliyoyapendekeza kocha huyo.
Habari za ndani zilizotufikia zinasema kwamba uongozi wa klabu hiyo, umeonyesha imani kubwa na kocha Mwambusi hivyo kumtaka kurejea tena kikosini.
Moja ya masharti ambayo yamewekwa bayana na kocha huyo kwamba ni lazima uongozi kuyatekeleza ni kwamba endapo atarejea kikosini asingependa uongozi kumuingilia kwenye majukumu yake ya kiutendaji.
Pia uongozi, huo umetakiwa kuweka mipaka kwa mashabiki ambao kwa sasa wameonekana kuitawala klabu hiyo hadi kufikia hatua ya kuingilia utendaji wa mwalimu kwa kumtaka kupanga wachezaji wanaowataka wao.
Akizungumzia hilo, Meya wa Jiji la Mbeya, Athanas Kapunga ambaye pia ni mwenyekiti wa bodi ya timu hiyo, amesema suala la kocha kujiuzulu bado linafanyiwa kazi na uongozi na kwamba vikao vya kulijadili bado vinaendelea kufanyika.
Mwambusi anaweza kurejea Mbeya City |
Hata hivyo masharti ya kocha huyo yametajwa kuwa huenda yakawagharimu baadhi ya viongozi. Imehamishwa kutoka http://www.jamiimoja.blogspot.com
0 comments:
Post a Comment