Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
BEKI wa Azam FC, Erato Edward Nyoni amepata ajali eneo la Kijitonyama, Dar es Salaam jioni ya leo, baada ya gari lake kugongana na pikipiki.
Walioshuhudia tukio hilo, wanasema mwendesha pikipiki aliingia vibaya barabarani na kugongana na gari la beki huyo kimataifa wa Tanzania.
Hata hivyo, baada ya tukio hilo, mwendesha bodaboda huyo aliwapigia simu wenzake na kumiminika kwa wingi eneo la tukio kwa ajili ya kumpiga mchezaji huyo.
Bahati nzuri, Erasto naye aliwahi kuwataarifu viongozi wa klabu yake, ambao walichukua hatua ya kumfuata haraka eneo la tukio ili kumtoa salama.
Hiyo inatokana na desturi moja mbaya ya waendesha bodaboda na bajaji Dar es Salaam kuchukua sheria mkononi baada ya ajali inayomuhusisha mwenzi wao, kumpiga kama mwizi aliyegongana naye, pasipo kujali nani alikuwa ana makosa.
Taarifa zaidi za tukio hilo zinatarajiwa kutolewa na jeshi la Polisi Kinondoni, Dar es Salaam kesho.
![]() |
Beki wa Azam, Erasto Nyoni |
Walioshuhudia tukio hilo, wanasema mwendesha pikipiki aliingia vibaya barabarani na kugongana na gari la beki huyo kimataifa wa Tanzania.
Hata hivyo, baada ya tukio hilo, mwendesha bodaboda huyo aliwapigia simu wenzake na kumiminika kwa wingi eneo la tukio kwa ajili ya kumpiga mchezaji huyo.
Bahati nzuri, Erasto naye aliwahi kuwataarifu viongozi wa klabu yake, ambao walichukua hatua ya kumfuata haraka eneo la tukio ili kumtoa salama.
Hiyo inatokana na desturi moja mbaya ya waendesha bodaboda na bajaji Dar es Salaam kuchukua sheria mkononi baada ya ajali inayomuhusisha mwenzi wao, kumpiga kama mwizi aliyegongana naye, pasipo kujali nani alikuwa ana makosa.
Taarifa zaidi za tukio hilo zinatarajiwa kutolewa na jeshi la Polisi Kinondoni, Dar es Salaam kesho.
![]() |
Gari la Erasto Nyoni baada ya kugongana na bodaboda |
0 comments:
Post a Comment