• HABARI MPYA

    Sunday, June 13, 2021

    BEKI WA KUSHOTO WA AKADEMI, PASCHAL MSINDO ASAINI MKATABA WA MIAKA MITATU TIMU YA WAKUBWA AZAM FC

    BEKI wa kushoto chipukizi wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Azam FC, Paschal Msindo amesaini mkataba wake wa kwanza rasmi wa miaka mitatu wa kuitumikia timu ya wakubwa ya klabu hiyo.
    Msindo aliyepandishwa timu kubwa kutokea timu yetu ya vijana (Azam FC U-20), ameshacheza mechi tatu za mashindano za Azam FC, akifanikiwa kuonyesha kiwango kizuri.
    Na kwa kusaini mkataba huo, Msindo ataendelea kusalia kwenye viunga vya Azam Complex hadi mwaka 2024.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BEKI WA KUSHOTO WA AKADEMI, PASCHAL MSINDO ASAINI MKATABA WA MIAKA MITATU TIMU YA WAKUBWA AZAM FC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top